*TUTAWATUMIKIA WANANCHI KAMA ILANI YETU INAVYOTUELEKEZA MADIWANI KISARAWE*
KISARAWE PWANI. Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Mhe. Aidan Kitale amewaasa Madiwani na watalamu wa Halmashauri kufanya kazi kwa weledi na bidii katika kuwatumikia wananchi wa Kisarawe ikiwa ni pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo sambamba na kutatua kero mbalimbali za Wanakisarawe
|
|
|
Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 03/12/2025 wakati wa kikao cha kwanza cha baraza la madiwani kwa mwaka 2025/2026 kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe,
“Nitoe rai kwa wataalamu wote na waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kufanya kazi kwa bidii bila kulegalega huku mkisimamia misingi ya utumishi wa umma kwa kufanya hivyo tutakuwa tunawatendea haki wananchi wetu wa Kisarawe “. Amesema Mhe.Kitale
Aidha Mhe. Kitale na baraza lake ameahidi kuboresha huduma mbalimbali za kijamii ikiwa ni pamoja na miundombinu ya afya , elimu , kilimo, na miundo ya barabara,
Akizungumza Mkuu wa Wilaya ndugu Petro Magoti amewataka waheshimiwa madiwani kwenda kufanya kazi kwani uchaguzi umeshapita kilichobaki na kwenda kufanya mikutano , kusikiliza na kutatua kero za Wananchi na serikali iko bega kwa bega kutoa ushirikiano.
Naye Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya Kisarawe Ndg Beatrice Dominic ametoa rai kwa madiwani kuwa watu wa kutoa huduma kwa wananchi wao lakini pia ameendelea kuwasisitiza watalamu wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kutumia utalamu wao kuwahudumia wananchi Ili kuijenga Kisarawe kimaendeleo.
Aidha ametoa mrejesho kwa baraza la madiwani kwa yale mambo ambayo waliyaacha hayajakamilikwa kuwa kwa sasa yametekelezwa kwa asilimia kubwa sambamabana kuendelea kufanya vizuri katika kukusanya mapato.
Nae Makamu Mwenyekiti wa baraza la Madiwani MHE Mbegu Rwambo amesema kuwa jukumu kubwa ni kuendelea kukusanya mapato na kuhakikisha mapato hayo yanakwendenda kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo huku akitoa kwa Wanakisarawe kuendelea kuilinda Amani kwani pasipo Amani hakuna maendeleo yanaweza kufanyika hivyo wananchi wote waaswa kwendelea kuilinda na kuidumisha Amani.
*"Ndugu zangu tunayafanya haya kwasababu tunaamnai, sisi tuliopo hapa twendelea kulinda na kudumissha Amani, tukapeleke ujumbe kwa watu wengine kuidumisha Amani tukakemee kwa nguvu kubwa , tukatae na kujiepusha na uvunjifu wa Amani kwani bila kuwa na Amani yote tuliyo panga kuyafanya hayawezi kutimia pasipo kuwa na Amani “ amesema Mhe. Rwambo
Kikao cha kwanza cha baraza la madiwani kimeenda sambamba na kuapishwa kwa madiwani, kuchagua mwenyekiti na makam mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na kupokea taarifa ya utekeleza wa shughuli mbalimbali zilizotekelezwa kipindi ambacho madiwani hawakuwepo Kisarawe.
Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa