• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kisarawe District Council
Kisarawe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazigira
      • Afya
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA NA UHUSIANO
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji na Nyuki
    • Programu
      • TASAF
      • UKIMWI
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
      • Vivutio vya Mali kale
      • Vivutio vya Utamaduni
      • Vivutio vya Asili
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Teknolojia
    • Industries
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
      • Huduma za Jamii
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba za Viongozi Mbali mbali

Mifugo na Uvuvi

IDARA YA MIFUGO NA UVUVI

TAARIFA YA IDARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA MWAKA 2017/18 

Idara ya Mifugo na Uvuvi inatekeleza shughuli mbalimbali za kitaalam ikiwa ni pamoja na utoaji huduma za ugani kwa wafugaji kwa kuwashauri kufuata kanuni za ufugaji bora na wenye tija wa mifugo ya aina tofauti, Pia idara inajishughulisha na utoaji ushauri wa kitaalam kuhusiana masuala ya uvuvi ikiwa ni pamoja na uvuaji samaki katika mabwawa. Ufugaji na uvuvi ni  mojawapo ya shughuli muhimu sana za kiuchumi ambazo husaidia wananchi kujiajiri na kuzalisha mifugo na samaki na mazao yake kama vile nyama, maziwa ,mayai, ngozi na  vifaranga vya samaki kwa ajili ya  kuuza na kujipatia kipato cha kumudu kuendesha maisha yao. Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ina jumla ya ng’ombe wa asili 45,899, ng’ombe wa maziwa 3564, mbuzi wa asili 9331, mbuzi wa maziwa 651, kondoo 1322, nguruwe 3148, mbwa 3289, paka 428, kuku wa asili 211176, kuku wa kisasa 65678, punda 21 na mabwawa ya samaki 24 mpaka hivi sasa.

  • MALENGO YA IDARA

Lengo kubwa ni kuhakikisha wafugaji wanapata elimu ya ufugaji bora wa kisasa na wenye tija kwa nia ya kumfanya mfugaji aongeze kipato ili aondokane na umaskini uliokithiri lakini pia kuongeza pato la taifa.

  • Idara imejiwekea malengo ya kutoa huduma bora za ugani ili kuwasaidia wadau wake kutekeleza kanuni za ufugaji wa kisasa na kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya mifugo na samaki ili kujiongezea kipato chao na pia kuboresha lishe katika ngazi ya kaya/familia na hatimaye wilaya.
  • MAFANIKIO
  • Idara imekuwa ikitekeleza kazi mbalimbali na kutoa ushauri kwa wadau wake kupitia huduma za ushauri na ugani kwa maafisa mifugo kuwashauri walioko vjijini kuwashauri wafugaji na wavuvi kufuata na kutumia mbinu za kisasa za uzalishaji kwa lengo kuongeza uzalishaji wa mazao bora ya mifugo na samaki ili kuwanufaisha wazalishaji. Mpaka hivi sasa wilaya imefanikiwa kutenga jumla ya hekta 63,442.84 katika jumla ya vijiji 24 vilivyofanyiwa mpango wa matumizi bora ya ardhi wilayani. Pia kuna maabara moja ya mtu binafsi ya kutotolesha vifaranga wa samaki aina ya pelage.
  • Pia kuna kituo kimoja cha uhimilishaji na kituo cha kutotolesha vifaranga katika kijiji cha Mloganzila 
  • CHANGAMOTO
  • Idara inazo changamoto kama ifuatavyo:-
  • Ufinyu wa bajeti ili kutekeleza majukumu na kazi mbalimbali za kila siku kama utoaji chanjo za mifugo na kichaa cha mbwa.
  •  Ukosefu wa usafiri kuwafikia wafugaji walioko mbali na kukwamisha ufuatiliaji ,
  • Ukosefu wa vitendea kazi kama veterinary kits, extension kits , protective gears.
  • Pia changamoto nyingine  ni ukosefu wa miundo mbinu ya mifugo katika maeneo yaliyotengwa kwa malisho hali inayochangia mifugo mingi kurundikana katika vijiji vilivyoko kando kando ya mto Ruvu hususan vijiji vilivyoko katika kata ya Mafizi.
  • Baadhi ya wafugaji kutokuwa tayari aidha kukinga au kutibu mifugo yao
  • Maduka ya madawa kutokuwa karibu na maeneo ya wafugaji hivyo inakuwa vigumu kupata dawa za kinga na matibabu zinapohitajika, pia gharama inakuwa kubwa pale wanapozifuata maeneo ya mijini kama vile Dar es Salaam.
  • Ukosefu wa machinjio ni changamoto kubwa katika sekta ya mifugo Wilayani.
  • Kutowepo kwa ulinzi madhubuti mnadani na hivyo kupelekea wafanyabiashara ya mifugo kukwepa kulipa ushuru na kusababisha mapato kidogo kukusanywa.
  • Wafugaji kutokuwa na vibanio (crashes) imara kwa ajili ya zoiezi la kupiga chapa hivyo kusababisha zoezi kutumia muda mrefu sana.
  • Upungufu au uhaba wa maji hususan kipindi cha kiangazi hali inayosababisha wafugaji kutafuta rasilimali hiyo katika maeneo mengine na kusababisha migogoro na wadau wengine

 





IKAMA YA IDARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

 

Aina ya Kada

Mahitaji

Waliopo

Mapungufu

LFO’s (Livestock Field Officer’s)

23

15

8

LO’s (Livestock Officer’s)

7

7

0

VO’s (Veterinary Officer’s)

1

1

0

TOTAL

31

23

8

MAJUKUMU KWA MPANGILIO WA IDARA YA MIFUGO NA UVUVI

JUKUMU (Role) 

WAJIBU (Responsibility) 

ENEO LA KIPAUMBELE (Area of focus) 

UENDELEZAJI SEKTA YA   MIFUGO NA UVUVI (W)
1.Kutafsiri sera, mikakati, miongozo na sheria mbalimbali za Kitaifa sanjari na hali halisi ya maendeleo ya uzalishaji wa mifugo na uvuvi Wilayani.
1.Kuhakikisha tafsiri sahihi  ya Sera zinazosimamiwa na Sekta ya Mifugo na uvuvi Wilayani

2.   Kuandaa maandiko ya mipango ya Maendeleo   Kilimo/Mifugo na Uvuvi (DADPs) kwa uwakilishi wa walengwa kwa
      mpango shirikishi.
2.  Kupata miradi sahihi
     itakayoweza kutatua
     kero za jamii.

3.Kuwezesha na kuwa
kiungo kati ya Taasisi za watafiti wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, wafugaji, wadau mbalimbali wa ngazi za Kata, Vijiji na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya.
3.  Mbinu za ufugaji bora
     zinawafikia wafugaji na
     pia matatizo na
     changamoto za ufugaji
     zinafikishwa kwa
     watafiti
     kwa kutafutiwa
     ufumbuzi.

4.Kusimamia miongozo
       ya kutoa huduma mbalimbali za mifugo kupitia sekta binafsi na mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali (NGOs) na CBOs), watoa huduma za mifugo na uvuvi kibiashara na kuwashirikisha, kuwahimiza watumie uwezo wao kutoa huduma za baadhi ya vyanzo vitakavyobinafsishwa ili kuendeleza huduma hizo Wilayani.
4.Kushirikisha wadau
       katika kutoa huduma za mifugo


5.Kuwajibika kuongoza na kuharakisha matumizi  sahihi ya pembejeo za mifugo zenye ruzuku ya serikali kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na kuhakikisha maamuzi sahihi yanafanyika haraka na kwa wakati kwenye zabuni 
5. Kuhakikisha ruzuku ya  pembejeo ya mifugo  zinawafikia na 
    kuwanufaisha wafugaji 
    kama ilivyokusudiwa na 
    Serikali. 

6.Kuhakikisha kuwepo kwa  mrejesho wa matokeo ya tafiti mbalimbali za mifugo kwa wafugaji na vikundi vya wafugaji Wilayani.
6.Kuhakikisha  tathmini na taarifa za utendaji kazi wa Idara zinatolewa.

7.Kuwa na mawasiliano
       kati ya Taasisi na Mashirika yanayojihusisha na mambo mtambuka ndani ya Wilaya kama vile: Maliasili, Jinsia, Mazingira na Mashirika ya uwezeshaji kimkoa kama RFAs kwenye masuala ya UKIMWI n.k ili kuona kwamba masuala hayo yanaingizwa kwenye mpango klazi ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Wilayani.


8.Kuratibu na kutoa        ushauri wa masuala ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi yanayotekelezwa Wilayani na Serikali pamoja na Mashirika binafsi.  Kufuatilia, kutathmini na kutoa taarifa za matukio ya majanga mbalimbali kama vile mlipuko wa wadudu wanaoshambulia mazao, magonjwa ya mifugo ya mlipuko n.k kwenye mamlaka za Kanda, Mkoa na Maafisa wa ngazi za Taifa na Idara husika  




Matangazo

  • Wito Kwenye Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari tarehe 10-11/02/2025 Minaki Sekondari. February 07, 2025
  • Tangazo kwa Umma Kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura February 08, 2025
  • MKITANO WA BARAZA LA MADIWANI April 28, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NOVEMBA 2021 November 09, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NIMEFURAHISHWA NA MMLIVYOJIPANGA KISARAWE CHATANDA NA ZAINABU

    May 08, 2025
  • OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS SERIKALI MAPINDUZI ZANZIBAR YAFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYA KISARAWE

    April 30, 2025
  • KISARAWE YAFANYA UTOAJI ELIMU YA DOZI YA NYONGEZA YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO(IPV2)

    April 30, 2025
  • KUVUNJWA KWA BARAZA LA MADIWANI KISARAWE UONGOZI WAJIVUNIA KUKAMILISHA MIRADI MBALIMBALI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 5

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Kamati ya Fedha kutembelea Ujenzi wa Jengo Jipya la OPD Kisarawe Hospitali
Video

Viungio

  • Utalii wa asili
  • Bima ya Afya (CHF)
  • Historia ya Kisarawe
  • Matukio mbali mbali ya Picha
  • Ukarabati wa Jengo la Upasuaji.
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Kukutana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Maelekezo jinsi ya kutumia Mfumo wa FFARS
  • Orodha ya Madiwani pamoja na Namba za simu

Viungio linganishi

  • OFISI YA RAIS UTUMISHI
  • Baraza la Mitiani ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
  • PPRA
  • Ikulu
  • Ajira
  • Idara kuu ya Takwimu
  • Tovuti ya kupata nakara ya Mshahara
  • Tovuti ya Taifa
  • Bunge
  • Mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST
  • Mfumo wa Upimaji Utendaji kazi wa Watumishi wa Umma (ESS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Kuhusu Sisi

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa