• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kisarawe District Council
Kisarawe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazigira
      • Afya
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA NA UHUSIANO
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji na Nyuki
    • Programu
      • TASAF
      • UKIMWI
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
      • Vivutio vya Mali kale
      • Vivutio vya Utamaduni
      • Vivutio vya Asili
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Teknolojia
    • Industries
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
      • Huduma za Jamii
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba za Viongozi Mbali mbali

Kilimo na Umwagiliaji

Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ina eneo lipatalo hekta  353 500, (3,535 Km2) ambapo eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta 380,000 kati ya hizo kiasi cha hekta 30 000 ndilo linalolimwa, (NBS, 2002).

Hali ya hewa

1.Hali ya mvua

Wilaya ya Kisarawe inapata mvua za aina mbili ( i ) mvua za muda mfupi yaani mvua za vuli  ambazo hunyesha muda mfupi  kuanzia mwezi Octoba na kuishia mwezi  Disemba na (ii ) mvua za muda mrefu yaani mvua za masika, mvua hizi huanza mwezi march na kuishia mwezi Juni. Wastani wa mvua zinazonyesha wilayani kwa mwaka  ni  mm 1,400 hadi mm 1,600  kwa upande wa mashariki wa wilaya ambayo ni maeneo ya tarafa ya Sungwi, na maeneo ya magharibi ambayo ni Chole na Mzenga yanapata mvua kidogo kiasi cha mm 1,000 kwa mwaka, (KDC, 2010).

Picha na. 1:      Kituo cha upimaji wa hali ya hewa Kisarawe

2   Nyuzi joto

Nyuzijoto ni kiwango cha ubaridi au joto la kitu husika mfano mwili wa binadamu. Eneo lipo katika mwiinuko wa mita 150 hadi 900 kutoka usawa wa bahari. Hivyo eneo lina nyuzijoto kati ya  280C hadi 330C kwa wastani wa nyuzijoto 30.50C.

Takwimu ya idadi ya watu,

Kutokana na sensa ya taifa ya idadi ya watu mwaka 2012 wilaya ilikuwa na idadi ya watu wapatao  101 598 na kiwango cha ukuaji wa watu ni wastani wa asilimia mbili pointi moja kwa mwaka  (2.1%). Inakadiriwa kuwa kiwango cha idadi ya watu kinaweza kufikia  108,472 ifikapo mwaka 2018. Idadi ya wanawake ilikuwa 50,967 Wanaume walikuwa 50,631 idadi ya kaya ilikuwa  26,051. Wastani wa ukubwa wa kaya moja ilikuwa ni 3.9, (KDC, 2017).

      Picha na. 2:          Ramani ikionyesha wilaya ya Kisarawe

 

KILIMO;

 

Wilaya ya Kisarawe ina eneo kubwa ambalo lina rutuba ya kutosha ya kuotesha mazao mbalimbali lakini eneo hili halijaweza kutumiwa vya kutosha na wakazi ili waweze kuzalisha chakula cha kutosha. Katika eneo lote linalofaa kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo asilimia saba nukta tisa ( 7.9%)  ndilo ambalo huwa linatumika,  (URT, 2007). Kwa wakazi wa wilaya ya Kisarawe asilimia tisini na tano (95%) ya wakazi hutegemea shughuli za kilimo kuendesha maisha. Wengi wao wakiwa ni wakulima wadogo wakijihusisha na uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. Zao kuu la biashara wilayani ni korosho, Muhogo ukiwa kama zao kuu la chakula na upande mwingine bisahara. Mazao mengine yanayolimwa ni mahindi, mpunga, mtama, ndizi, viazi vitamu, nazi na mbogamboga. Pia wilaya inafursa ya mazao mengine yakiwemo matunda kama vile Embe, Machungwa, Fenesi, Passion, Nanasi na “Citrus”, (KDC, 2017). Soko kubwa la mazao yanayozalishwa wilaya ya Kisarawe ni Dar es salaam and Kibaha.

MNYORORO WA THAMANI WA ZAO LA MUHOGO

 

Mhogo ndio zao kuu la chakula na pia zao la biashara na ni zao lililochaguliwa na Halmashauri kama ni zao la mnyororo wa thamani la Wilaya. Zao hili linakabiliwa na tatizo la kushambuliwa na magonjwa ya batobato (CMD) na michirizi ya kikahawia(CBSD); kwa hali hiyo Halmashauri imehakikisha uwepo wa ubora wa zao la muhogo kupitia uliokuwa Mradi wa kushirikisha Jamii kutambua na kupunguza maambukizi ya magonjwa ya mhogo (Cassava Community Phytosanitation Project). 

Kisarawe ni moja kati ya wilaya 4 ambazo zimetekeleza mradi huo. Wilaya nyingine ni Chato, Muleba na Mkuranga. Katika kutekeleza hilo kumeanzishwa mashamba darasa matatu katika Kijiji cha Mhaga kwa kupandwa mbegu bora ya mhogo yaani Kibaha 026 (KBH O26) na Kiroba kutoka kituo cha utafiti Kibaha (SRI) zenye ukinzani na maambukizi ya magonjwa ya batobato na michirizi ya kikahawia. Katika mradi huo wakulima walipata fursa ya mafunzo mbalimbali kuhusiana na kilimo cha mhogo kwa kutumia mbegu zisizo na maambukizi ya magonjwa ya batobato na michirizi ya kikahawia na namna ya kupunguza maambukizi. Pamoja na mashamba darasa 3 ya ekari moja kila moja kwa kila kitongoji na shamba la mbegu ekari 5 bado mahitaji ya mbegu ya mhogo kwa wakulima ni makubwa maeneo mengi ya wilaya yameathirika na magonjw hayo. Kwa sasa wilaya ina mpango wa kuhamasisha  jamii ili  kila Kata kuwepo na Kijiji kimoja kitakachokuwa  na Kikundi kitakachopata mafunzo kuhusiana na zao la mhogo na kusimamia shamba la mbegu na hatimaye kuweza kuwa na mbegu isiyo na maambukizi ya kutosheleza na kusambaza mbegu hiyo kwenye vijiji vingine vya Kata husika kwa gharama nafuu.

 

Picha na. 3.:   Wataalam wakilimo na baadhi ya wakulima wakiwa wametembelea shamba darasa la Mhogo

Picha na. 4:            Shamba darasa la mhogo kijiji cha Mhaga lililopandwa mbegu aina ya Kibaha 026


Picha na. 5:            Shamba la mbegu ya Mhogo lililopandwa mbegu aina ya Kibaha026 

Vilevile mradi umeweza kuwaelimisha wakulima namna ya usindika zao la mhogo kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali na kuweza kujiongezea kipato.

Picha na. 6:    Wakulima kijiji cha Mhaga wakiwa kwenye mafunzo ya usindikaji


Picha na. 7:            Siku ya wakulima Kijiji cha Mhaga. Wanakukundi wakionyesha bidhaa zitokanazo na Mhogo

ZANA ZA KILIMO

Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe katika kutekeleza Mipango ya Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya (District Agricultural Development Plans – DADPs) imeweza kuviwezesha Vijiji kwa kuvipatia zana za kilimo aina mbalimbali. Maudhui makuu ya kuwepo kwa zana hizi ni  kuongeza mnyororo wa thamani wa zao la muhogo.

Zana za kilimo zilizosambazwa vijijini ni pamoja na matreka makubwa manane (8), Vituo vya usindikaji wa zao la muhogo tisa (9), mashine za kuchakata muhogo kumi na mbili (12), mashine za usindikaji wa mazao ya mafuta tatu (03), na  matrekta ya mkono (powertiller) ishirini na nne (24).

MATREKTA MAKUBWA.

Matrekta makubwa manane yaliyopo yalikabidhiwa Vikundi ambavyo viliteuliwa na Kijiji kupitia Mikutano Mikuu ya Vijiji husika. Kati ya matrekta hayo manane, manne yalinunuliwa na kumilikiwa na Vikundi vya Usindikaji wa muhogo vya Kisanga, Zegero, Mhaga, na Kidugalo Chakanga. Matrekta mengine manne yalikabidhiwa Vikundi vya uzalishaji wa mazao ya kilimo katika Vijiji vya Kwala, Kazimzumbwi, Msimbu na Marui Mgwata.

VITUO VYA KUSINDIKA ZAO LA MUHOGO

Vituo tisa vya kusindika zao la muhogo vinakamilishwa kuwepo kwa vifaa maalum vikiwemo jengo, trekta, mashine ya kuchakata muhogo “Crater”, mashine ya kutengeneza chips “Cheaper”, Mashine ya kusaga muhogo   “Milling machine”  na mashine ya kukamulia muhogo uliochakatwa “Pressor mashine”.

  • Vituo vyenye ukamilifu wa vifaa hivyo ni vinne (04) ambavyo ni Kisanga, Zegero, Mhaga, na Kidugalo Chakanga.
  • Vituo vitatu (03) havina trekta kutokana na fedha za kukamilisha mradi kutopokelewa hadi kipindi program ya Mpango wa Kuendeleza Kilimo awamu ya pili ilipomalizika mwaka 2014/15 ambavyo ni vya Luhangai, Chole na Vihingo.
  • Kituo cha Mitengwe hakina banda kutokana na fedha za kujengea banda kubadilishiwa matumizi na kutumika kumalizia jengo la soko la Mitengwe.
  • Kituo cha Sungwi kina mashine ya kuchakata muhogo na mashine ya kusaga.

MASHINE ZA KUCHAKATA NA KUKAMULIA MUHOGO

Mradi huu ulinunuliwa vifaa vya mashine ya kuchakata muhogo “Crater”, na mashine ya kukamulia muhogo uliochakatwa “Pressor mashine”.

Vijiji kumi na mbili (12) vilivyowezeshwa kununuliwa mashine za kuchakata muhogo ni vijiji vya Gumba, Kibuta, Mtamba, Maguruwe, Chang’ombe B, Bembeza, Titu, Kihare, Chole, Kazimzumbwi, Mhaga, na Marumbo. 

MASHINE ZA USINDIKAJI WA MAZAO YA MAFUTA

Vijiji vitatu vya Vikumburu, Mfuru na Kikwete vina mashine za usindikaji wa mafuta kama ifuatavyo:-

  • Vikumburu -    Mashine za Usindikaji wa mazao ya mafuta ya alizeti, karanga, mbegu za maboga, mbegu za matikiti  na Ufuta.
  • Mfuru na Kikwete       -           mashine za kusindika mafuta ya mawese

MATREKTA YA MKONO (POWERTILLERS).

Matrekta ya mkono (powertiller) ishirini na nne (24) yakiwemo matatu yaliyopo kwenye vituo vya kilimo vya Kibuta, Mafumbi na Mzenga. Vijiji vilivyonufaika na zana hizi ni Mzenga, Mafizi, Nyani (2), Mianzi, Vihingo, Kurui, Marumbo, Msanga, Maneromango, Chole, Marui, Vikumburu, Msimbu, Kisarawe, Kibuta Masaki, Kiluvya, Mitengwe.

Picha na. 8:     Kikundi cha Mshikamano (Wanawake ) cha uchakataji muhogo cha  wa kijiji cha  Kitanga 


Picha na.9.:     Trekta la Kikundi cha Mshikamano (Wanawake ) cha uchakataji muhogo cha  wa kijiji cha  Kitanga 

 

                                         

 

VITUO VYA KILIMO  (Ward Agricultural Resource Centre -  WARCs)

Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo  (Agricultural Sector Development Programme - ASDP) ilibuni mradi wa Kujenga Vituo vitatu vya Rasilimali ya Kilimo vya Kata (Ward Agricultural Resource Centre -  WARCs) katika Kata za Mzenga, Kibuta na Chole (Mafumbi).

Utekelezaji wa Mradi huu ambao ulifanyika kwa awamu, ulianza katika mwaka wa fedha 2010/11 ambapo kiasi cha Shilingi 72,000,000/= zilipokelewa kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa vituo. Awamu ya pili katika mwaka wa fedha wa 2014/15 Halmashauri ilipokea shilingi 330,000,000/= ambazo zilitumika kumalizia ujenzi wa vituo, maandalizi ya mashamba darasa, kununulia samani, Kompyuta, jenereta na Trekta 3 za mikono aina za power tiller.

Kwa mujibu wa Mwongozo wa kuanzisha na kuendesha Vituo vya Rasilimali za Kilimo vya Kata (Ward Agricultural Resource Centre – WARCs)  wa mwaka 2008 Ukamilifu wa Vituo hivi ni kuwepo kwa eneo la kutosha kati ya hekta 1-2  litakalowezesha kukamilishwa kwa mambo yafuatayo:-

Kuwepo kwa Jengo la Ofisi lenye Chumba cha nafasi ya kutosheleza wataalam angalau sita wa Kilimo, Mifugo na Ushirika, ukubwa wa kutosheleza kuweka kompyuta angalau sita; Chumba cha maktaba kwa ajili ya kutunza vitabu, majarida na taarifa mbalimbali na kiwe na ukubwa wa nafasi inayoruhusu angalau watu 15 kujisomea kwa wakati mmoja; Chumba cha mikutano na mafunzo chenye uwezo wa kuchukua angalau watu 40 kwa wakati mmoja; Maabara ndogo itakayowezesha kufanya uchunguzi wa awali wa sampuli za mimea, mifugo na kutunza dawa za chanjo na kutoa huduma ya Uhimilishaji (Artificial Insemination); na Stoo inayotosheleza kuhifadhi vifaa na pembejeo.

Kuandaa mashamba ya maonesho kwa ajili ya mafunzo na yanayoendeshwa kibiashara.

Maliwato: bafu na  choo chenye matundu manne yanayozingatia jinsi

Banda/karakana ya kuhifadhia zana za kilimo na mifugo;

Kibanio cha mifugo (cattle crush).

Mabweni mawili (me na ke) ya kutosha watu 20 kila moja kwa ajili ya malazi ya wakulima wakati wa mafunzo yatakayolazimu kulala kituoni;

Jukumu la Halmashauri ya Wilaya ni  kuwezesha katika ujenzi, vifaa, habari na teknolojia.

Mambo ya msingi yaliyokwisha fanyika ni upatiknaji wa eneo la kutosha katika kila kituo, ujenzi wa Ofisi zenye kukidhi haja, maeneo ya shamba darasa, ununuzi wa vifaa/zana za kilimo (matrekta ya mkono), samani na maliwato zimejengwa. Mahitaji mengine (iv – vi) bado kukamilishwa. Aidha bado kukamilishwa Maabara ndogo na Stoo.

Kutokana na mapungufu hayo makubwa Vituo hivi bado kukamilika.

  • Utaratibu wa usimamizi na uendeshaji wa WARCs :-
  • Kamati ya Uendeshaji (Steering Committee) ya WARCs ndiyo ambayo inasimamia shughuli za uendeshaji. Mtendaji Kata ni Mwenyekiti na Afisa Kilimo wa Kata ni Katibu. Pamoja na hao Kamati hii inajumuisha wawakilishi wa vikundi, NGO/CBO, Wataalam wa, Maendeleo ya Jamii, Misitu nk. na wajumbe wasizidi 10. Uwakilishi wa jinsia na vijana unatakiwa uzingatiwe wakati wa utekelezaji wa kuunda Kamati..
  • Makabidhiano ya Vituo vya Mzenga na Kibuta yamefanyika bado Kituo cha Mafumbi.

WARCs za Mafumbi, Kibuta na Mzenga katika mwaka wa 2014/15 zilianza kutoa mafunzo katika kipindi cha masika kama ifuatavyo:-.

  • Kituo cha Kibuta
  • Shamba la maonesho kwa kilimo cha mazao ya kudumu (miembe na michungwa) na shamba la maonesho ya mazao aina mbalimbali ya msimu  ya mihogo, viazi, karanga. Mazao ya bustani kama vitunguu, pilipili hoho na karoti yalilimwa kama Shamba la maonesho ili wakulima waweze kujifunza kupitia vipando hivyo.
  • Kituo cha Mzenga
  • Shamba la maonesho kwa kilimo cha mazao ya msimu kilifanyika kwa mazao ya ufuta na mahindi.
  • Kituo cha Mafumbi
  • Shamba la maonesho kwa kilimo cha mazao ya msimu kilifanyika kwa zao la mahindi lakini kutokana na ukosefu wa walinzi yalishambuliwa na wanyama waharibifu.

Mafunzo hayo yalitolewa bila ya kuwepo kwa bajeti ya Halmashauri ikiwa ni juhudi binafsi za Ma afisa Ugani wa maeneo husika.

Aidha Vituo vya kilimo hufanya kazi nyingine zikiwemo za walengwa kutembelea vituo na kupata mafunzo kupitia maandiko ya kilimo bora cha mazao mbalimbali ambapo pia huweza kuazimwa vitabu hivyo. Pia kumbi zilizopo zinatumika kuendeshea mafunzo pale ambapo yanapopata mgharamiaji. Shughuli nyingine za ugani zilizoendeshwa kwa mwaka 2015/16 (kiangazi) ni kama zifuatazo:-

  • Kituo cha Kibuta
  • Wanakikundi 50 wa Kikundi cha Kilimo na ufugaji cha Kijiji cha Mloo walifanya ziara ya mafunzo ya upandaji na uchakataji wa mhogo
  • Kikundi cha Mpunga Bwama kilifanya ziara Kituoni na kuazima maandiko ya kilimo bora cha mpunga
  • Wakulima binafsi 72 kutoka Vijiji jirani walitembelea Kituo kuona shamba darasa la miembe na michungwa.
  • Mafunzo ya Wahudumu 20 wa mashine za kupulizia mikorosho kutoka Tarafa za Sungwi na Maneromango yalifanyika kituoni.
  • Kituo cha Mzenga na Mafumbi
  • Wakulima binafsi kutoka Vijiji jirani walitembelea Vituo kwa lengo la kusoma na kuazima maandiko mbalimbali yahusuyo kilimo bora.
  • Kwa kipindi cha masika ya msimu wa 2015/16 kazi zilizofayika katika Vituo ni kuandaa mashamba ya maonesho katika vituo vya Kibuta na Mzenga. Vipando vilikauka kutokana na changamoto ya hali ya hewa ya kutokuwepo kwa mvua za kutosha

Changamoto:-

Pamoja na Vituo kuanza kutoa mafunzo vilikuwa na changamoto zifuatazo:-

  • Hakukuwepo na bajeti ya kuendesha Vituo hivyo kwa mwaka 2014/15 na 2015/16
  • Hakuna maji ya bomba/ visima
  • Changamoto ya hali ya hewa ya kutokuwepo kwa mvua za kutosha

Matarajio 2016/17

Kwa mwaka huu 2016/17 Halmashauri imeweka bajeti ya sh. 2,384,788/= Kwa kila Kituo kwa ajili ya mbegu na pembejeo. Fedha hizi zinatarajiwa kutokana na bajeti ya miradi ya maendeleo zitakazopatikana kutoka mapato ya ndani (own source).

Picha Na 10:   Kituo cha kilimo cha kata ya Kibuta.



Picha Na 11:   Mafunzo ya uanzishaji vitalu vya miche bora ya korosho Kibuta.

 

 

 

Takwimu za uzalishaji mazao;

Aina ya zao 
2007/08
2008/09
2009/10
2010/11
2011/12
2012/13
2013/14
Muhogo

66,857

63,036.4

240.9

10,045

25,772.4

8,340

36,450

Mahindi

814.5

7,506

1,208.2

1,444.6

1,278.2

4,306

3,454

Mtama

2,290

1,610

35.8

48

900

610

261

Mpunga

8,500

722

891.3

110

365

1,069

590.4

Mikunde

4,603

3,493.5

197.8

568.6

975.8

1,120

178.1

Viazi vitamu

6,000

34,200

3,170.7

355.5

3,650

1,326

1,380

Jumla

89,064.5

110,567.9

5,744.7

12,571.7

32,941.4

16,771

42,313.5

Jedwali na 1. Takwimu ya uzalishaji ( kwa tani)  2007 – 2014.

 

Picha Na 12:   Maafisa kilimo walipomtembelea mkulima wa mpunga kijiji cha Kihare


Picha Na 13:   Shamba darasa la zao la nyanya eneo la  Kisarawe Nanenane mjini Morogoro.

 

TAKWIMU YA UZALISHAJI WA MATUNDA   2007 – 2014

 

Aina ya zao
2007/08
2008/09
2009/10
2010/11
2011/12
2012/13
2013/14
Machungwa

657

692

1,140

1,148

1,158

1,158

1,158

Embe

1,163

1,165

1,166

1,173

1,173

1,182

1,190

Nazi

7,680

7,810

7,992

7,998

8,753

8,753

8,760

Chikichi

1,251

1,370

1,270

1,370

1,370

1,370

1,370

Korosho

975.64

1,050

1,150

1,300

28

810

670

Jumla

11,726.64 

 12,370

12,718

12,989

12,482

13,273

13,148

 

Jedwali na. 2: Takwimu ya uzalishaji wa matunda Kisarawe

 

Picha Na 14:   Shamba la miembe kata ya Kurui 

 

 

UMWAGILIAJI; 

Wilaya ya Kisarawe ina maeneo makubwa yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji yapatayo hekta 5,000 kati ya hizo hekta 40 ndizo ambazo zipo chini ya maandalizi kwa ajilia ya umwagiliaji eneo hilo lipo kijiji cha Mianzi kata ya Msanga.

Wilaya imepanga kutumia eneo la umwagiliaji kwa kuchukua maji kutoka katika mto kwa kutumia miundombinu yenye thamani ipatayo 3,600,000,000 pesa za kitanzania. Utekelezaji wa mpango huu unatarajiwa kuanza pindi pesa itakapopatikana.

Maeneo ambayo umwagiliaji unaweza kufanyika kisarawe.

s/n

Scheme

Start of farmland

 

Intake site

Latitude

longitude

Latitude

longitude

1.

Mafizi
E.038.56096o
S.06.99986o
E.038.55953o
S.07.000660

2.

Marui – Mipera (Mtuna bwawani)
E.038.767260
S.07. 354870
E.038.767350
S.07.354110

3.

Marui – Mipera (Mkongoroni)
E.038.765170
S.07.343820
E.038.7653380
S.07.343910

4.

Marui – Ngwata (kisoti bwawani)
E.038785180
S.07.380670
E.038.785770
S.07.380690

5.

Mianzi
E.038.781730
S.07.305290
E.038.781530
S.07.304500

6.

Nyani
E.038.538400
S.07.051730
E.038.531890
S.07.049270

Jedwali na. 3: Takwimu za Maeneo ambayo umwagiliaji unaweza kufanyika kisarawe

Maeneo mengine sita yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji ambayo hayajafanyiwa uhakiki ni Gwata, Ving’andi, Bwama Doloto, Kimalamisale na Mihugwe.

Matangazo

  • Wito Kwenye Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari tarehe 10-11/02/2025 Minaki Sekondari. February 07, 2025
  • Tangazo kwa Umma Kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura February 08, 2025
  • MKITANO WA BARAZA LA MADIWANI April 28, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NOVEMBA 2021 November 09, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NIMEFURAHISHWA NA MMLIVYOJIPANGA KISARAWE CHATANDA NA ZAINABU

    May 08, 2025
  • OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS SERIKALI MAPINDUZI ZANZIBAR YAFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYA KISARAWE

    April 30, 2025
  • KISARAWE YAFANYA UTOAJI ELIMU YA DOZI YA NYONGEZA YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO(IPV2)

    April 30, 2025
  • KUVUNJWA KWA BARAZA LA MADIWANI KISARAWE UONGOZI WAJIVUNIA KUKAMILISHA MIRADI MBALIMBALI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 5

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Kamati ya Fedha kutembelea Ujenzi wa Jengo Jipya la OPD Kisarawe Hospitali
Video

Viungio

  • Utalii wa asili
  • Bima ya Afya (CHF)
  • Historia ya Kisarawe
  • Matukio mbali mbali ya Picha
  • Ukarabati wa Jengo la Upasuaji.
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Kukutana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Maelekezo jinsi ya kutumia Mfumo wa FFARS
  • Orodha ya Madiwani pamoja na Namba za simu

Viungio linganishi

  • OFISI YA RAIS UTUMISHI
  • Baraza la Mitiani ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
  • PPRA
  • Ikulu
  • Ajira
  • Idara kuu ya Takwimu
  • Tovuti ya kupata nakara ya Mshahara
  • Tovuti ya Taifa
  • Bunge
  • Mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST
  • Mfumo wa Upimaji Utendaji kazi wa Watumishi wa Umma (ESS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Kuhusu Sisi

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa