• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kisarawe District Council
Kisarawe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazigira
      • Afya
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA NA UHUSIANO
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji na Nyuki
    • Programu
      • TASAF
      • UKIMWI
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
      • Vivutio vya Mali kale
      • Vivutio vya Utamaduni
      • Vivutio vya Asili
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Teknolojia
    • Industries
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
      • Huduma za Jamii
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba za Viongozi Mbali mbali

MHE. JAFO ATEMBELEA UJENZI WA SEKONDARI YA KISARAWE ILIYOPO KATA YA KAZIMZUMBWI PAMOJA NA KUONGEA NA WATUMISHI KATIKA HALMASHAURI YA KISARAWE.

Posted on: December 28th, 2020

MHE. JAFO ATEMBELEA UJENZI WA SEKONDARI YA KISARAWE ILIYOPO KATA YA KAZIMZUMBWI PAMOJA NA KUONGEA NA WATUMISHI KATIKA HALMASHAURI YA KISARAWE.

Kisarawe ,Pwani

28/12/2020

Leo tarehe 28/12/2020 Mara baada ya Mapumziko ya sikukuu ya Krismass Mhe Jafo afanya ziara ya kukagua ujenzi wa shule ya Sekondari Kisarawe ambayo inajengwa kwenye kata ya Kazimzumbwi.Mara baaada ya kuwasili Mhe waziri alipokea taarifa fupi toka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ndugu Musa Gama kuhusu hatua za ujenzi zilipofikia na taarifa ya upokeaji wa wanafunzi wa kidato cha kwanza.Ndugu Gama alisema mpaka sasa hakuna mwanafunzi aliyefaulu atakayekosa nafasi ya kujiunga kidato cha kwanza.Katibu Tawala ndugu Mwanana alimkaribisha Mhe. Jafo ili kuongea machache kisha kuelekea eneo la Shule inapojengwa. Katika ukaguzi huo Mhe. Waziri Jafo aliwapongeza wanaosimamia ujenzi kwa kufikia hatua nzuri. Hata hivyo Mhe. Jafo aliwasisitiza waongeze kasi ya ujenzi ili ifikapo tarhe 11/01/2021 ujenzi uwe umekamilika na wanafunzi waanze kutumia majengo hayo. Mpaka sasa ujenzi unaendelea kwa kujenga Madarasa,maabara,ofisi za walimu ,Bwalo la chakula,Chumba cha TEHAMA na Jengo la Utawala.

Mhe Jafo ameridhishwa sana na hatua hiyo na kuwaagiza watendaji na Wanakijiji kutoa ushirikiano na kulinda mali zote zinazotumika katika ujenzi wa shule hiyo.

Aidha wakati Mhe. Jafo akiongea na wananchi aliwatoa hofu kwa kuwaambia kuwa shule hiyo ni maalumu kwa watoto wa kisarawe na sio watoto kutoka Mikoa mingine.

Pamoja na ziara ya kukagua ujenzi wa shule ya sekondari kisarawe Mhe Jafo ambaye pia ni mbunge wa kuchaguliwa na wananchi Kupitia chama cha Mapinduzi alipata nafasi ya kuongea na  watumishi wa Taasisi za Umma mbalimbali pamoja na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya kisarawe.

Kwanza aliwashukuru watumishi kwa kumchagua kuwa Mbunge wao pia kumshukuru Mhe.Rais John Magufuli kwa kumchagua kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Baada ya shukrani hizo Mhe Jafo alitoa maelekezo yafuatayo:

  1. Kuhakikisha Halmashauri inakusanya mapato na kuziba mianya yote ya upotevu wa mapato.
  2. Kuhakikisha Hospitali yetu ya kisarawe pamoja na vituo vyetu vya kutolea Huduma zinatoa Huduma nzuri huku ikitumia mifumo ya kukusanya Mapato.
  3. Kuhakikisha walimu wa shule za msingi na sekondari kufanya kazi na kukaa karibu na shule.
  4. Kuhakikisha watumishi wa Afya kukaa karibu ya vituo vya kutolea huduma ili kurahisisha utoaji wa huduma pindI inapohitajika kwa dharura.
  5. Kuboresha Soko letu la kisarawe liwe soko la kisasa kila kitu kiwe kinapatikana hapo hili sambamba na kuboresha stendi na kuhakikisha mabasi yote ya kwenda nje ya kisarawe yanapatikana.
  6. Watumishi wafanye kazi kwa kujiamini na kupendana bila kujali cheo.

Mwisho Mhe Waziri Jafo alitoa pole kwa msiba wa baba yake Mzazi Mhe. Mkuu wa Wilaya Jokate na kuwashukuru kwa kushiriki hatua zote hadi kumpumzisha Marehemu huko Mbinga.Waziri aliwataka watumishi wanapoanza mwaka 2021 wakaanze na nguvu mpya wakisahau changamoto zote za mwaka 2020.

Sambamba na hilo Mwenyeki wa chama cha Mapinduzi Ndugu Sika aliwashukuru watumishi kwa kufanya vizuri kwenye kazi zao na kuwataka waendelee na kuongeza bidii huku wakipunguza maneno yasiyoleta maendelee kwa wilaya yetu.

Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri ndugu Zuberi Kizwezwe alimshukuru Mhe.Jafo kwa kuja kuongea na watumishi na kuahidi kuwa yote aliyoyaelekeza atakwenda kuyasimamia na kuhakikisha yanatekelezeka.Pia alisema atatoa ushirikiano wa kutosha kwa watumishi ili kufikia malengo chanya ya Halmashauri.

Picha zaidi bofya hapa

Imetolewa na Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO(W)

Kisarawe.

Matangazo

  • Wito Kwenye Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari tarehe 10-11/02/2025 Minaki Sekondari. February 07, 2025
  • Tangazo kwa Umma Kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura February 08, 2025
  • MKITANO WA BARAZA LA MADIWANI April 28, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NOVEMBA 2021 November 09, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NIMEFURAHISHWA NA MMLIVYOJIPANGA KISARAWE CHATANDA NA ZAINABU

    May 08, 2025
  • OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS SERIKALI MAPINDUZI ZANZIBAR YAFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYA KISARAWE

    April 30, 2025
  • KISARAWE YAFANYA UTOAJI ELIMU YA DOZI YA NYONGEZA YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO(IPV2)

    April 30, 2025
  • KUVUNJWA KWA BARAZA LA MADIWANI KISARAWE UONGOZI WAJIVUNIA KUKAMILISHA MIRADI MBALIMBALI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 5

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Kamati ya Fedha kutembelea Ujenzi wa Jengo Jipya la OPD Kisarawe Hospitali
Video

Viungio

  • Utalii wa asili
  • Bima ya Afya (CHF)
  • Historia ya Kisarawe
  • Matukio mbali mbali ya Picha
  • Ukarabati wa Jengo la Upasuaji.
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Kukutana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Maelekezo jinsi ya kutumia Mfumo wa FFARS
  • Orodha ya Madiwani pamoja na Namba za simu

Viungio linganishi

  • OFISI YA RAIS UTUMISHI
  • Baraza la Mitiani ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
  • PPRA
  • Ikulu
  • Ajira
  • Idara kuu ya Takwimu
  • Tovuti ya kupata nakara ya Mshahara
  • Tovuti ya Taifa
  • Bunge
  • Mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST
  • Mfumo wa Upimaji Utendaji kazi wa Watumishi wa Umma (ESS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Kuhusu Sisi

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa