• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kisarawe District Council
Kisarawe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazigira
      • Afya
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA NA UHUSIANO
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji na Nyuki
    • Programu
      • TASAF
      • UKIMWI
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
      • Vivutio vya Mali kale
      • Vivutio vya Utamaduni
      • Vivutio vya Asili
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Teknolojia
    • Industries
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
      • Huduma za Jamii
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba za Viongozi Mbali mbali

'Mkaa Ni Gharama,Tumia Nishati Mbadala'

Posted on: June 4th, 2018

Mazingira ni jumla ya mambo na vitu vyote vinavyomzunguka kiumbe hai.Hii inamaanisha kuwa kila kitu kinachomzunguka kiumbe hai na kinachosababisha uwepo na uendelezaji wa uhai ni mazingira.

Viumbe hai vinategemea mazingira,hata viumbe visivyo hai pia hutegemea mazingira yaani inajumuisha ardhi ,maji,hewa uoto, na vinginevyo ambapo kwa umoja wake unasababisha uhai uwepo na uendelee.Kwa misingi hii ni wajibu wetu kupambana kuhifadhi na kulinda mazingira endapo tunahitaji kuishi na kuendeleza uhai kwa vizazi vijavyo.

Juhudi tunazoziimarisha na kuamsha ari kubwa miongoni mwetu kwa  wanajamii katika kulinda mazingira kunaakisi umuhimu na tija katika maendeleo ya viwanda.

Madhara makubwa ya kuendelea kuharibu mazingira yetu na athari zitokananzo na uharibifu huu zinafanya jamii zetu zipate maumivu ambayo yanasababishwa na sisi wenyewe kutokana na  ukosefu wa maarifa, ujinga na kutojali ingawa athari zake hazihitaji kutumia darubini kutambua kuwa tumetafuta majanga haya wenyewe.

Tujiulize kwa nini watu wanaharibu mazingira? Kitu gani kinasababisha tuharibu mazingira yetu? Je ni jinai kuharibu mazingira yetu ? Ukweli usiojificha  ni kuwa  ukataji wa miti usiozingatia sheria ni mwiba mchungu kwa maendeleo ya taifa hili.

Takwimu zinaonyesha kuwa kwa siku moja zaidi ya  ekari elfu kumi (10,000) zinaharibiwa kwa ajili ya matumizi ya mkaa na matumizi mengine hapa nchini. Asilimia tisini (90%) ya watanzania wanatumia mkaa ambapo asilimia themanini na tano (85%) ya matumizi ya mkaa huo hutumiwa na wakazi wanaoishi jijini Dar es Salaam.

Zipo sababu zinazofanya watanzania wengi watumie nishati ya  mkaa na baadhi yake ni utamaduni na mazoea . Mazoea katika kutumia nishati ya mkaa huamini kuwa mkaa huivisha chakula vizuri kama maharage,wali nk.kulinganisha na nishati ya gesi au umeme.mazoea/utamaduni  haya hupelekea hata watu wenye kipato cha kati kupendelea kutumia nishati hii japo inaharibu mazingira.

Sababu nyingine inayochangia watu waendelee kutumia nishati ya mkaa ni nguvu ya soko (biashara) ambapo soko la mkaa ni jepesi na ni rahisi kuiendesha kulingana na mazingira yetu na pia ni rahisi kwa gharama kulinganisha na nishati nyinginezo jambo ambalo si la kweli kiuhalisia

Kipato duni ni sababu nyingine kwani nishati mbadala imeonekana ni ghali sana hali hii hupelekea watu wengi kutumia mkaa na ukweli ni kwamba kipato cha watanzania wengi hasa wale wa maeneo ya ya vijijini ambao ndio watumiaji wakubwa wakubwa wa nishatiya kuni na mkaa.

Pamoja na sababu zote zilizoorodheshwa zinazosababisha ukataji wa mkaa bado sisi kama wana mazingira hatuziafiki na hatukubaliani nazo, kwani zipo njia nyingi na rahisi ambazo tukitumia tunaweza kutimiza mahitaji yetu na pia kulinda mazingira.

Njia rahisi ni kutumia nishati mbadala.Nishati ambazo haziwezi kuharibu mazingira na zimependekezwa na wanamazingira na wataalamu kuwa zinafaa.Nishati hizo zaweza kuwa Nishati ya gesi, Nishati ya jua (Solar power), Umeme, Bayogesi (nishati inayotokana na uozo wa masalia mbalimbali ya vyakula na hata vinyesi vya wanyama) na nishati ya mkaa unaotokana na masalia ya uchafu/takataka za nyumbani mfano vifuu vya nazi,pumba za mbao,maganda ya korosho na mabunzi ya mahindi.

Napenda kunukuu kauli ya mwalimu ambaye pia alikuwa ni Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Julius Nyerere kuwa ‘’Elewa  kuna kitu kinaitwa wizi,wizi wote ni mbaya,lakini wizi mbaya kupita wote ni kumuibia mtoto wako ambaye hajazaliwa,ni kumuibia mjukuu,unaiba mali yake.Na kuharibu mazingira ni kuiba mali ya vizazi ambavyo havijazaliwa.Wewe umekuta mlima ule una miti mizuri,umerithishwa wewe na wale waliokutangulia,wamekupa mazingira mazuri ya miti yana miti mizuri,inaleta hewa nzuri na inasaidia kuleta mvua.Wewe kwa ujinga wako unaharibu miti ile,watoto wako na wajukuu wako wanaokuja baadae wanakuta hali si nzuri kama uliyokuwa nayo,Umewaibia!Mwizi weye!Mwizi! Tupande miti!!’’

Mikakati yetu wanamazingira,hasa tunaotoka maenea ambayo yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira hasa unaotokana na mkaa .Sisi wana wa Kisarawe Mkoa wa Pwani tumeazimia kutoa elimu kwa jamii kuhusu athari za matumizi ya mkaa,uundaji wa vikundi vidogo vidogo vya mazingira katika vitongoji na mashuleni na kamati ndogo za moto za vijiji.

Pia kuweka mikakati ya pamoja kwa kushirikiana na taasisi nyinginezo mfano TFS,WWF,Wizara ya Nishati na Madini NG’Os na CBO’s na kufanya makongamano mbalimbali katika kuhamasisha jamii juu ya matumizi bora ya nishati mbadala.

Kuwatambua wadau wanaotoa mchango wa kutunza na kuhifadhi mazingira kiwilaya ili kuweza kushirikiana nao katika shughuli mbalimbali za simamizi na uhifadhi wa mazingira ikiwezekana kuwapa  motisha.

Halmashauri kushirikiana na wizara yenye dhamana ya mazingira na maliasili kuyatambua na kutenga maeneo ya hifadhi ili kunusuru uoto na ikolojia yake isiendelee kuharibiwa.

By dkambanyuma

 

 

Matangazo

  • Wito Kwenye Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari tarehe 10-11/02/2025 Minaki Sekondari. February 07, 2025
  • Tangazo kwa Umma Kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura February 08, 2025
  • MKITANO WA BARAZA LA MADIWANI April 28, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NOVEMBA 2021 November 09, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NIMEFURAHISHWA NA MMLIVYOJIPANGA KISARAWE CHATANDA NA ZAINABU

    May 08, 2025
  • OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS SERIKALI MAPINDUZI ZANZIBAR YAFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYA KISARAWE

    April 30, 2025
  • KISARAWE YAFANYA UTOAJI ELIMU YA DOZI YA NYONGEZA YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO(IPV2)

    April 30, 2025
  • KUVUNJWA KWA BARAZA LA MADIWANI KISARAWE UONGOZI WAJIVUNIA KUKAMILISHA MIRADI MBALIMBALI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 5

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Kamati ya Fedha kutembelea Ujenzi wa Jengo Jipya la OPD Kisarawe Hospitali
Video

Viungio

  • Utalii wa asili
  • Bima ya Afya (CHF)
  • Historia ya Kisarawe
  • Matukio mbali mbali ya Picha
  • Ukarabati wa Jengo la Upasuaji.
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Kukutana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Maelekezo jinsi ya kutumia Mfumo wa FFARS
  • Orodha ya Madiwani pamoja na Namba za simu

Viungio linganishi

  • OFISI YA RAIS UTUMISHI
  • Baraza la Mitiani ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
  • PPRA
  • Ikulu
  • Ajira
  • Idara kuu ya Takwimu
  • Tovuti ya kupata nakara ya Mshahara
  • Tovuti ya Taifa
  • Bunge
  • Mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST
  • Mfumo wa Upimaji Utendaji kazi wa Watumishi wa Umma (ESS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Kuhusu Sisi

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa