• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kisarawe District Council
Kisarawe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazigira
      • Afya
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA NA UHUSIANO
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji na Nyuki
    • Programu
      • TASAF
      • UKIMWI
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
      • Vivutio vya Mali kale
      • Vivutio vya Utamaduni
      • Vivutio vya Asili
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Teknolojia
    • Industries
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
      • Huduma za Jamii
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba za Viongozi Mbali mbali

NMB Yakabidhi Madawati Wilaya Ya Kisarawe

Posted on: August 16th, 2018

NMB Yakabidhi Madawati Wilaya Ya Kisarawe

Benki ya NMB Tanzania imekabidhi madawati mia moja  katika Wilaya ya Kisarawe kwa ajili YA Matumizi kwa shule mbili za Sekondari ya Masaki na Mfuru zilizopo Wilaya ya Kisarawe.

Katika makabidhiano hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari vya Masaki na Mfuru  Mkurugenzi wa masuala ya serikali wa benki ya NMB bi………….alimkabidhi madawati Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mheshimiwa Jokate Mwegelo  amesema Benki ya NMB imeweka kipaumbele kushirikiana na serikali kutatua changamoto mbalimbali zinazokabili jamii.

‘’Tulipopata maombi yenu,tulifarijika na kuamua mara moja kuja kushirikiana na ninyi ili kuwa chachu ya maendeleo katika sekta ya elimu.Madawati tunayokabidhi leo ni moja ya ushiriki wetu katika maendeleo ya jamii na sisi kama benki inayoongoza Tanzania tunahakikiksha jamii inafaidika kutokana na faida tunayopata.Benki ya NMB imekuwa ikishiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kama vile kusaidia sekta ya elimu  afya pamoja na kufariji jamii katika vipindi mbalimbali kama mafuriko,matetemeko na ajali mbalimbali zinazogusa jamii’’Amesema Bi Aneth Kwaya 

Wakati akipokea Msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mheshimiwa Jokate Mwegelo ameishukuru benki ya NMB kwa msaada huo ambao utakuwa chachu kubwa kwa matokeo mazuri kwa wanafunzi .Pia aliwaasa wanafunzi kusoma kwa bidii na kuleta matunda 

‘’Zero haikubaliki,hatuitaki zero! Hatuongei tu bali tunamaanisha,Walimuwanafanya kazi nzito kuwafundisha,serikali inafanya kazi ya kipekee na benki ya NMB ikaona iweke mkono wake ili kuwabariki wanafunzi ili mazingira yenu ya kusoma yawe mepesi. Kwa hiyo ninyi kama wanafunzi mna deni zito sana la kulipa na deni hilo mtalilipa pale tu mtakapofanya vizuri darasani na kufaulu’’ Amesema Mheshimiwa Jokate.

Katika makabidhiano hayo Benki ya NMB imekabidhi jumla ya madawati mia moja yenye jumla ya thamani ya shilingi milioni tano ambapo shule ya Sekondari ya Masaki imepata madawati hamsini na Shule ya sekondari ya Mfuru imepata madawati hamsini.

Hafla ya makabidhiano pia imehudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani wa Kata ya Masaki na  Marumbo  Mhe.Pili Chamgui na Mhe.Mayasa S. Yange, Katibu Tawala wa Kisarawe Ndugu Mtela Mwampamba,Kaimu Mkurugenzi Ndugu Patric  Allute,Afisa elimu Sekondari bi Generosa Nyoni na Maafisa wa Benki ya NMB Tawi la Kisarawe wakiongozwa na Meneja wa benki hiyo Ndugu Sumka 

Matangazo

  • Wito Kwenye Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari tarehe 10-11/02/2025 Minaki Sekondari. February 07, 2025
  • Tangazo kwa Umma Kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura February 08, 2025
  • MKITANO WA BARAZA LA MADIWANI April 28, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NOVEMBA 2021 November 09, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NIMEFURAHISHWA NA MMLIVYOJIPANGA KISARAWE CHATANDA NA ZAINABU

    May 08, 2025
  • OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS SERIKALI MAPINDUZI ZANZIBAR YAFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYA KISARAWE

    April 30, 2025
  • KISARAWE YAFANYA UTOAJI ELIMU YA DOZI YA NYONGEZA YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO(IPV2)

    April 30, 2025
  • KUVUNJWA KWA BARAZA LA MADIWANI KISARAWE UONGOZI WAJIVUNIA KUKAMILISHA MIRADI MBALIMBALI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 5

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Kamati ya Fedha kutembelea Ujenzi wa Jengo Jipya la OPD Kisarawe Hospitali
Video

Viungio

  • Utalii wa asili
  • Bima ya Afya (CHF)
  • Historia ya Kisarawe
  • Matukio mbali mbali ya Picha
  • Ukarabati wa Jengo la Upasuaji.
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Kukutana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Maelekezo jinsi ya kutumia Mfumo wa FFARS
  • Orodha ya Madiwani pamoja na Namba za simu

Viungio linganishi

  • OFISI YA RAIS UTUMISHI
  • Baraza la Mitiani ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
  • PPRA
  • Ikulu
  • Ajira
  • Idara kuu ya Takwimu
  • Tovuti ya kupata nakara ya Mshahara
  • Tovuti ya Taifa
  • Bunge
  • Mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST
  • Mfumo wa Upimaji Utendaji kazi wa Watumishi wa Umma (ESS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Kuhusu Sisi

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa