• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kisarawe District Council
Kisarawe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazigira
      • Afya
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA NA UHUSIANO
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji na Nyuki
    • Programu
      • TASAF
      • UKIMWI
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
      • Vivutio vya Mali kale
      • Vivutio vya Utamaduni
      • Vivutio vya Asili
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Teknolojia
    • Industries
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
      • Huduma za Jamii
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba za Viongozi Mbali mbali

Tutimize Wajibu Wetu ‘TUSIPOE’

Posted on: June 7th, 2018

Sheria ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2010 ilipitishwa na bunge la Jamhuri ya Muugano wa Tanzania mwezi april 2010 na kusainiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 20 mei 2010.

Tujiulize?  Hata kwa sauti tuwaze!  Ni nani haswa anayepaswa kusimamia sheria hii? Je ni bunge ambalo ndio waliotunga sheria hii? Je ni serikali au Mahakama ambayo kisheria na kimamlaka ndio wasimamizi wakubwa wa sheria zetu tunazozitunga? au ni jamii ambayo tunaguswa na changamoto hizi au ni walemavu? NINI TUFANYE?

Kwanza sisi  tukiwa jamii inatupasa tutambue tangu awali viashiria  vya utambuzi wa watoto wenye ulemavu,Hii itasaidia kuweza  kujua mapema athari zilizopo na pengine kuweza kuepuka au kupunguza athari kwani baadhi ya matatizo ya ulemavu yanaweza kutibika  na kuepukika iwapo utambuzi utafanyika mapema  kwa watoto.

Ulemavu ni hali inayotokana na upungufu katika viungo vya mwili,vya akili na milango ya fahamu ambayo inampunguzia mtu uwezo na fursa hasa hali hiyo inapokutana na vikwazo katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali katika jamii.

Katika hali ya kuthaminiana,kujali utu na heshima ya mwanadamu ambapo watanzania ndiyo jadi yetu, suala linalotugusa jamii bila kujali itikadi,rangi kabila wala imani tunapaswa kuwajibika kwa pamoja na sio suala la kuwaachia taasisi,asasi, kikundi au serikali kuwajibika katika kulinda na kutetea maslahi ya kundi Fulani lenye mahitaji bali ni sote kwa pamoja.

Sheria ya watu wenye ulemavu imewekwa ikiwa na lengo la kuweka mwongozo wa kisheria wa namna ya utekelezaji utoaji huduma kwa watu wenye ulemavu,kujenga uelewa wa pamoja miongoni mwa wanajamii juu ya haki za watu wenye ulemavu na kuchangamana na kushirikiana katika mazingira mbalimbali ya kazi ,kijamii na fursa za kiuchumi,

Pia kukuza uelewa miongoni mwa jamii juu ya wajibu na majukumu ya kila mwananchi na mamlaka mbalimbali za kijamii kuhakikisha haki na fursa za watu wenye ulemavu zinaimarishwa ili kujenga jamii jumuishi inayowakubali watu wa aina zote.

Mara nyingi kunapotokea tukio la kuwakutanisha pamoja watu wenye ulemavu na wale wasio walemavu ni dhahiri jamii ya wasio na ulemavu tumeshuhudia wakisononeshwa na kuhuzunishwa na hali waliyo nayo walemavu.Basi kama ndivyo, huzuni hii isiwe inaishia kwa kuwaonea huruma tu bali pia itukumbushe wajibu wetu wana jamii jukumu la kuhakikisha tunawahudumia , kushirikiana na kuchangamana nao si kwa sababu sheria imetaka iwe hivyo bali ni hiari ya lazima ya kutimiza wajibu wetu kutoka ndani ya mioyo yetu .(nafsi zetu) 

Nafsi zetu zitukumbushe kuwa tuna wajibu wa kukomesha ubaguzi na kuleta usawa,wajibu wa kutoa msaada wa kijamii kwa watu wenye ulemavu,wajibu wa kuwalinda na wajibu wa kutoa ajira na kuendeleza ajira kwa watu wenye ulemavu.

Katika kutekeleza wajibu na matakwa ya sheria hii inatupasa sote kwa pamoja tuwajibike huku tukiwa na furaha mioyoni mwetu kwa tendo la kishujaa tunalofanya kama ilivyo kwa baadhi ya taasisi.asasi na serikali inavyawajibika katika hili.

Mfano Hai,Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe iliyopo Mkoa Pwani imedhamiria na kuanza kutekeleza wajibu wake kwa kuwapatia watu wote wenye ulemavu Wilaya ya Kisarawe bima ya afya ambayo itawawezesha walemavu kupata matibabu bure kwenye Zahanati,Vituo vya afya na Hospitali zilizopo Wilaya ya Kisarawe.  

Kitendo hiki kitapunguza mzigo mzito waliokuwa nao walemavu katika kugharamia huduma ya matibabu kwani kama tunavyojua gharama za matibabu ni ghali sana si kwa walemavu pekee bali hata kwa watu walio na utimamu wa viungo na akili.

Kwa kuhitimisha napenda kunukuu kauli ya mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya walemavu Tanzania SHIVYAWATA bi Ummy Nderiananga kama ifuatavyo’’Niwageukie wenzangu wenye ulemavu,kwa vipawa tulivyojaaliwa na mwenyezi mungu naomba tujitaidi kuzichangamkia  fursa zilizopo katika maeneo yetu.Nawatia moyo nikiwaambia kuwa tunaweza, sisi viongozi wenu tupo pamoja nanyi’’

SISI tunawapenda,tunawajali na kuwalinda .Ndugu zangu, walemavu wasioona,viziwi,walemavu wa ngozi,walemavu wa akili,viungo, wagonjwa wa akili,walioumia uti wa mgongo na walemavu wa Mbalanga mbalanga Chepechepe tunawapenda, tuchangamkie fursa zilizopo mbele yetu kwani nguvu zenu kwa umoja wenu ni chachu kwetu jamii nzima ya Watanzania .  

By  dkambanyuma

 

 

  

Matangazo

  • Wito Kwenye Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari tarehe 10-11/02/2025 Minaki Sekondari. February 07, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA-AWAMU YA PILI TAREHE 16-22 MEI 2025 May 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NOVEMBA 2021 November 09, 2021
  • KUITWA KWENYE SEMINA YA ANUANI ZA MAKAZI March 30, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • JIMBO LA KISARAWE LATOA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • JIMBO LA KISARAWE LATOA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • JIMBO LA KISARAWE LATOA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • JIMBO LA KISARAWE LATOA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Kamati ya Fedha kutembelea Ujenzi wa Jengo Jipya la OPD Kisarawe Hospitali
Video

Viungio

  • Utalii wa asili
  • Bima ya Afya (CHF)
  • Historia ya Kisarawe
  • Matukio mbali mbali ya Picha
  • Ukarabati wa Jengo la Upasuaji.
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Kukutana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Maelekezo jinsi ya kutumia Mfumo wa FFARS
  • Orodha ya Madiwani pamoja na Namba za simu

Viungio linganishi

  • OFISI YA RAIS UTUMISHI
  • Baraza la Mitiani ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
  • PPRA
  • Ikulu
  • Ajira
  • Idara kuu ya Takwimu
  • Tovuti ya kupata nakara ya Mshahara
  • Tovuti ya Taifa
  • Bunge
  • Mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST
  • Mfumo wa Upimaji Utendaji kazi wa Watumishi wa Umma (ESS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Kuhusu Sisi

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa