• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Kisarawe District Council
Kisarawe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazigira
      • Afya
    • Vitengo
      • Sheria
      • TEHAMA NA UHUSIANO
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji na Nyuki
    • Programu
      • TASAF
      • UKIMWI
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
      • Vivutio vya Mali kale
      • Vivutio vya Utamaduni
      • Vivutio vya Asili
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Teknolojia
    • Industries
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
      • Huduma za Jamii
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba za Viongozi Mbali mbali

Watu Wenye ULemavu Wapatiwa Msaada Wa Vifaa saidizi

Posted on: May 21st, 2018

Watu wenye ulemavu wilaya ya kisarawe wamekabidhiwa msaada wa vifaa saidizi vyenye jumla ya kiasi cha shilingi milioni arobaini ambavyo vitawasaidia katika kupambana na changamoto mbalimbali zilizokuwa zina waathiri katika ufanisi wa ushiriki wao kwenye shughuli mbalimbali  za kiuchumi na kijamii.S

Katika zoezi hilo ambapo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa (TAMISEMI)  Mhe. Selemeni Jafo amekabidhi vifaa hivyo kwa watu wenye ulemavu tukio lililofanyika kwenye uwanja wa stendi kuu ya Wilaya ya Kisarawe. Walemavu wamepatiwa wheel chairs 40,Trycicle 15 na white canes 100.

Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi, Mwenyekiti wa SHIVYAWATA Taifa ndugu Ummy Nderiananga amesema baada ya kuwapa vifaa watu wenye ulemavu, tusogee mbele kuwakwamu kiuchumi.Pia aliwaasa watu wenye ulemavu kutumia vipawa walivyojaaliwa na mwenyezi mungu kuzichangamkia fursa zilizopo kwenye maeneo yao .

Aidha bi Ummy amemwambia mgeni rasmi kuwa Mradi huu wa kutoa vifaa visaidizi kwa watu wenye ulemavu ulipatikana mwaka 2017 na ni wa thamani was kiasi cha shilingi milioni mia mbili unatekelezwa kwa awamu mbili ,awamu ya kwanza ni Mkoa wa Dar es salaam na Pwani na awamu ya pili ni Mkoa wa Morogoro na Dodoma na una lengo la kuwafikia watu wenye ulemavu wapatao 2050 msaada utakaojumuisha Try cicle 150,Wheelchairs 350 na white Canes 1550 na mpaka sasa mradi umefanikiwa kuwafikia wanufaika 695 wakiwemo wa Wilaya ya Kigamboni,Ilala,Temeke,Ubungo na Kinondoni jijini Dar es salaam.

Wakati anahutubia hadhara iliyojitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo mgeni rasmi Mbunge wa Kisarawe ambaye pia ni Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI amesema kuwa jamii kwa ujumla inatambua changamoto walizonazo watu wenye ulemavu na inawathamini kwa mchango mkubwa unaotolewa na watu hao.

‘’Serikali inatambua na kuthamini mchango na juhudi kubwa zinazofanywa na watu wenye ulemavu,na tumekuwa na viongozi wengi wenye ulemavu ambao wamepata fursa ya kulitumikia Taifa katika Nyanja mbalimbali kwa ufanisi mkubwa na bado Serikali inaendelea kuwajali na kuwatambua kwa mchango wao.Hivi karibuni Serikali imetangaza ajira zaidi ya elfu sita kwenye sekta ya afya na ninawaahidi watu wote wenye ulemavu kuwa wenye sifa wote wataajiriwa kwa asilimia mia moja,pamoja na  ajira upande wa elimu wote kwa pamoja wataajiriwa’’ amesema Mhe. Selemani Jafo.

Katika zoezi hilo ambalo pia lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Evarist Ndikilo,Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mhe.Happiness Seneda , Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani Mhe. Zainabu vulu, Katibu tawala ndugu Mtela Mwampamba, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Mhe.Hamisi Dikupatile ,madiwani na Wataalamu wa Halmashauri wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Mussa Gama pamoja na wananchi waliojitokeza kwa wingi.                                                                      By dkambanyuma.

Matangazo

  • Wito Kwenye Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari tarehe 10-11/02/2025 Minaki Sekondari. February 07, 2025
  • Tangazo kwa Umma Kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura February 08, 2025
  • MKITANO WA BARAZA LA MADIWANI April 28, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NOVEMBA 2021 November 09, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NIMEFURAHISHWA NA MMLIVYOJIPANGA KISARAWE CHATANDA NA ZAINABU

    May 08, 2025
  • OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS SERIKALI MAPINDUZI ZANZIBAR YAFANYA ZIARA YA KIKAZI WILAYA KISARAWE

    April 30, 2025
  • KISARAWE YAFANYA UTOAJI ELIMU YA DOZI YA NYONGEZA YA CHANJO YA SINDANO YA POLIO(IPV2)

    April 30, 2025
  • KUVUNJWA KWA BARAZA LA MADIWANI KISARAWE UONGOZI WAJIVUNIA KUKAMILISHA MIRADI MBALIMBALI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 5

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Kamati ya Fedha kutembelea Ujenzi wa Jengo Jipya la OPD Kisarawe Hospitali
Video

Viungio

  • Utalii wa asili
  • Bima ya Afya (CHF)
  • Historia ya Kisarawe
  • Matukio mbali mbali ya Picha
  • Ukarabati wa Jengo la Upasuaji.
  • Mikakati ya Halmashauri
  • Kukutana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Maelekezo jinsi ya kutumia Mfumo wa FFARS
  • Orodha ya Madiwani pamoja na Namba za simu

Viungio linganishi

  • OFISI YA RAIS UTUMISHI
  • Baraza la Mitiani ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
  • PPRA
  • Ikulu
  • Ajira
  • Idara kuu ya Takwimu
  • Tovuti ya kupata nakara ya Mshahara
  • Tovuti ya Taifa
  • Bunge
  • Mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST
  • Mfumo wa Upimaji Utendaji kazi wa Watumishi wa Umma (ESS)

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Kuhusu Sisi

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe. Haki zote zimehifadhiwa